Jumanne, 26 Novemba 2013

SERIKALI YA WANAFUNZI WA DACICOSTUA 2013 WAKIAPISHWA

WAZIRI WA ELIMU JACKSON  YOHANA MOLELI
KATIBU MKUU-ROZINA MCHOMVU
NAIBU WAZIRI WA KATIBA, SHERIA, ULINZI NA USALAMA-SAULO SANASIO
WAZIRI MKUU-GOODLUCK MOSES KAJUNA
WAZIRI WA AFYA NA MAZINGIRA-RAZACK MUSHI
WAZIRI WA HABARI, MAMBO YA NDANI NA NJE-DIGNER CHUWA
WAZIRI WA KATIBA, SHERIA, ULINZI  NA USALAMA- CHRISTOPHER LYOGELO
WAZIRI WA MICHEZO, STAREHE NA MAAFA-ALEXZANDER NGELEZI

Jumatatu, 25 Novemba 2013

DACICO VS GLOBAL- ZATAMBIANA TEGETA

 Baadhi ya Wachezaji wa DACICO FC, wakiwa kwenye maandalizi ya mchezo huo
  Baadhi ya Wachezaji wa GLOBAL  FC, wakiwa kwenye maandalizi ya mchezo huo
 KIKOSI CHA GLOBAL FC
 KIKOSI CHA DACICO FC
 Wachezaji wa Timu wa DACICO  Vs GLOBAL, wakichuana Vikali katika mpambano huo.
 Baadhi ya Mashabiki wa DACICO wakifuatilia kwa makini mpambano
 Nyota wa DACICO, Said(mbele) akimtoka kiungo mchezeshaji wa GLOBAL, Moland, wakati wa mpambano
 Beki nyota wa timu ya DACICO FC, Mathias Canal, akijaribu kuondoa hatari zote kwenye lango la DACICO.
 Baadhi ya Mashabiki wa Timu ya Global Publishers, wakifuatilia kwa makini mpambano huo.
==================================================
Na: Wanafunzi DACICO.

imu ya Chuo cha Uandishi wa Habari na Utawala, Dar es Salaam City College(DACICO TANZANIA, mwishoni mwa juma ilicheza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Global Publishers, katika Uwana wa Shule ya Sekondari Tegeta.
Katika Mchezo huo ambao Global ilionekana kuzidiwa kwa kiwango kikubwa, hadi timu zote zinakwenda mapumziko matokeo ilikuwa 0-0 kabla ya timu Zote kufanya mabadiliko ya Hapa na pale, ambapo Global ilibidi kuwatumia wachezaji wa kukodi(Mamruki) na kuweza kuibuka na ushindi wa bao 1-0.
Akizungumzia mchezo huo, kocha wa timu ya DACICO FC, Ombeni, alisema kuwa kikosi chake pamoja na kupoteza mchezo huo ilitokana na wachezaji wengi kucheza bila mazoezi kutokana na kwamba muda mwingi waliutumia katika masomo kwani walikuwa katika maandalizi ya mitihani.
"tumefungwa na Global kwa mengi moja ni pamoja na kukosa mazoezi wachezaji wangu kutokana na kuwa kwenye maandalizi ya mitihani, pia wenzetu wa Global wametumia wachezaji Mamruki ambao siyo waajiliwa wao kama tulivyotarajia wangecheza wenyewe, wametuchezeshea wachezaji wa ligi sijui wamewachukua timu gani hawa maana wana kasi na mbio sana, lakini goli hilo moja tutarejesha wakati wa mchezo wa marudiano"alisema ombeni
mchezo mwingine wa marudiano unatarajia kuchezwa mwishoni mwa mwezi wa kumi na mbili.

Jumamosi, 16 Novemba 2013

BENDERA YA DACICO YAPANDISHWA RASMI MAKAO MAKUU YA CHUO DAR ES SALAAM.

Hii ndiyo Bendera ya Dar es Salaam City College  DACICO TANZANIA.
 Mkurugenzi Mkuu wa DACICO, Idrisa Mziray, Baada ya kukabidhi majukumu ya Bendera ya Chuo na ya Tanzania, ambazo zimepandishwa Rasmi Makao Makuu ya DACICO jijini Dar es Salaam.
 Mmoja wa Wafanyakazi wa DACICO-TANZANIA. Mpalule Shaaban, akipandisha Bendera ya Chuo Rasmi.
 Bendera ya DACICO ikiwa imepandishwa Tayari.

 Mkurugenzi Mkuu wa DACICO-TANZANIA, Bwana, Idrisa Mziray, muda mfupi baada ya Bendera ya DACICO Kupandishwa.
Majengo ya Chuo yakiwa katika Mwonekano wa Pekee baada ya Kupandishwa Bendera ya Chuo.(Picha Zote kwa Hissan ya Miss Demokrasia Tanzania).

Jumatano, 6 Novemba 2013

WANAFUNZI DACICO WAENDELEA NA MITIHANI KATIKA CUMPUS YA DAR, MBEYA NA SUMBAWANGA.

Baadhi ya Wanafunzi wa DACICO, Wakiwa katika Vyumba vya Mitihani Leo tarehe 6/11/2013, Cumpus ya Dar es Salaam.
Baadhi ya Wanafunzi wa DACICO, Cumpus ya Dar es Salaam, Muda mfupi kabla ya kuanza mitihani, wakisimama kwa ajili ya kupata Maombi.(Picha Zote kwa Hisani ya Miss Demokrasia Tanzania).

Jumamosi, 2 Novemba 2013

DACICO TANZANIA Diploma Vs Certificate, Zashindwa kutambiana.

Mwamuzi wa Mchezo huo Shaaban Mpalule, akionekana kuwaita baadhi ya wachezaji wa Timu zote kutokana na kuonyesha mchezo mbaya.(Picha na Mathias Haule).
 Baadhi ya Wanafunzi na Mashabiki wa Certificate, wakifuatilia kwa makini Mpambano huo
 Wachezaji wa Timu ya Certificate, wakielekeza mashambulizi katika lango la timu ya Diploma.
 Mashabiki wa timu hizo wakimzonga Mwamuzi baada ya kutaka kumlazimisha baadhi ya maamuzi wakati wa kupuliza filimbi, kitendoo kilichosababisha mpira kusimama kwa muda.
 Mchezaji Nyota wa Timu ya Certificate, Deogratius, akiambaa na mpira kuelekea katika lango la timu ya Diploma
 Mwamuzi wa Mpambano huo Shaaban Mpalule, akionyesha kati baada ya timu ya Certificate kusawazisha bao, ambalo hata hivyo lilitaka kuleta mzozo kutokana na wachezaji wa timu ya Diploma kugomea bao hilo ambalo liliunganishwa kwa mkwaju mkali baada ya kumshinda mlinda mlango wa timu ya Diploma.
Baadhi ya Matukio ya picha wakati wa mchezo huo(Picha zote na Mathias Haule).
======================================================
DIPLOMA Vs CERTIFICATE ZASHINDWA KUTAMBIANA.

Na: Mariam Mwakatumbula

Timu ya Soka ya DACICO Diploma dhidi ya timu ya Certificate jana zimeshindwa kufungana baada yab kutoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1 katika mchezo wa marudiano uliofanyika katika Uwanja wa Kibwegele nje kidogo ya mji wa Kibamba Chama.
Wakicheza mbele ya Mkurugenzi mkuu wa Chuo bwana Idrisa Mziray, wachezaji wa timu zote walionekana kucheza kwa kukamiana kutokana na kila mmoja kutaka kuchaguliwa katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo ambayo inatarajia kumenyana na timu za vyombo vya habari zikiwemo timu za Taswa F.c.
aidha katika mchezo wa kwanza uliochezwa kwenye Uwanja wa chuo cha DACICO uliopo kibamba CCM timu hizo zilishindwa kutambiana baada kumaliza dakika 90 kwa kufungana 2-2 na hivyo kuomba mchezo wa marudiano ambao pia timu hizo zimeshindwa kupata mbabe na kulazimisha kutafutwa mchezo mwingine ili iweze kujulikana ni timu ipi yenye ubavu itakayowezakuibuka na ushindi.
wakizungumza baada ya mpambano huo makocha wa timu zote mbili, Mwalimu Kashilima wa Diploma na Mwalimu wa Michezo wa Timu ya Certificate Ombeni  wamesema kuwa kushindwa kupata timu iliyoibuka na ushindi kumetokana na wachezaji kucheza kwa kukamiana na hivyo kusababisha mchezo huo kutawaliwa na vurugu zilizosababisha mwamuzi kushindwa kuumudu vyema mchezo huo kutokana na kila mara wachezaji kwenda kwa mwamuzi na kumzongazonga.
"Wachezaji wangu wamecheza mpira mgumu sana leo na hiyo imetokana na kukamia mpambano, unajua timu hizi ni pinzani pamoja na kwamba wanasoma katika chuo kimoja, kikubwa hapa ni kwamba wachezaji wa Diploma wanawaona hawa wa Certificate kama watoto wadogo, lakini kumbe mpira ama mchezo wowote hauna kuzarau, kwani hawa vijana wangu wa Certificate wanacheza mchezo mzuri na wa hali ya juu ila kwa leo naweza kusema wamecheza mchezo wan kuwaiga hawa wachezaji wa timu ya Diploma, ila tunaomba mchezo wa tatu ambao bila shaka utamaliza ubishi wote na hapo tutapata kufahamu ni timu ipi bora ukilinganisha na ingine" alisema mwalimu wa michezo katika chuo cha Uandishi wa habari na Utawala DACICO.
wakati huo huo kocha wa Diploma mwalimu kasilima amewalaumu wachezaji wa timu yake kwa kushindwa kulinda goli ambalo lilifungwa mapema kwenye dakika za mwanzo kabla ya kwenda mapumziko baada ya mchezaji nyota wa timu hiyo Hilary Mgenzi kuwalamba chenga walinzi wa timu ya Certificate na kisha kufunga kwa Shutin kali lililokwenda moja kwa moja wavuni na kumuacha mlinda mlango wa Certificate othman juma akiutazama kwa macho.
"sikutarajia kama mchezo huu ungekuwa mgumu kiasi hiki, maana hii ni mara ya pili tunashindwa kuibuka na ushindi pamoja na kwamba sisi ndiyo tunaanza kuwafunga hawa wenzetu wa Certificate, nilijaribu kuwapa maelekezo kuhusu kucheza kwa makini lakini kutokana na kukamia mchezo wachezaji wangu wameshindwa kufuata maelekezo yangu na hivyo kupelekea kusawazisha kwa hawa wachezaji wa Certificate, lakini tunazungumza na Mkurugenzi wetu ili aweze kudhamini mpambano mwingine utakaotoa matokeo ya timu ipi ni bora zaidi ya mwingine, mchezo ambao utakuwa ni wa mwisho kwa ajili ya kupata kikosi cha timu ya DACICO F.C. alisema Kasilima.
kwa mujibu wa mkurugenzi mkuu wa chuo bwana Idrisa Mziray, mchezo wa marudiano umepangwa kufanyika mapema baada ya wanafunzi kumaliza mitihani ambayo inatarajia kuanza jumatatu ya kwanza ya mwezi huu.