Jumatatu, 1 Septemba 2014

MASHAUZI CLASIC YAITIKISA- NAWINA RESORT MBAGALA KUU.

Na: Violet John.
(DACICO TANZANIA).

Wakazi wa Mbagala Kuu na Maeneo ya jirani, mwishoni mwa juma na mwishoni mwa mwezi huu Bendi ya Muziki wa Taarabu ,Mashauzi classic, chini yake, Aisha Mashauzi, siku ya juzi jumamosi tarehe 30/8/2014 katika Ukumbi wa Kisasa wa Nawina Resort uliopo Mbagala kuu  ilipowapa raha Mashabiki kwa kibao kipya cha Asiyekujua Akuthamini.
Mwimbaji nyota wa muziki wa Mwambao, Bi, Aisha Mashauzi, akipagawisha katika Ukumbi wa Nawina Resort.

Safu yetu ilipata kuongea
 na Meneja wa Mashauzi Classic Bw. Ismail Rashid (Suma Ragar) baada ya kushindwa kuzungumza na Aisha Mashauzi kutokana na hali yake kutokuwa nzuri.

Ismail Rashid alisema kuwa malengo makubwa ya bendi hiyo ni kuwapa watu ajira, kumiliki vitendea kazi, na kujiendeleza kimuziki .
Aidha pia alisema kwamba kwa sasa tayari wamekamilisha nyimbo kadhaa zinazotarajiwa kuingizwa hivi karibuni kwenye soko la muziki.
Nyimbo zinazotarajiwa kuingizwa sokoni ni pamoja na Sura siyo Roho, ulioimbwa na Isha Ramadhani, Wema hauuzwi na Ubaya haulipizwi, ulioimbwa na Asia Hamisi Mzinga.
Vile vile alisema kuwa katika bendi ya Mashauzi kuna waimbaji thelathini na mbili(32), ambao ni Isha Ramadhani ambaye pia ndiye mkurugenzi katika bendi hiyo , Rukia Juma ambaye  ni mama mzazi wa Isha, Hashimu Saidi, Zubeida Malicky,Abdulmali Shakani Malicky pamoja na Wengineo.

Mwimbaji nyota wa muziki wa Mwambao, Bi, Aisha Mashauzi, akipagawisha katika Ukumbi wa Nawina Resort.

“Na vile vile napenda kuwakumbusha mashabiki wetu kuwa kila alhamisi tunakuwa pale Mango Gareden Kinondoni kwa ajili ya kuwaburudisha mashabiki wetu kwa kiingilio cha shilingi elfu tano tu” alisema Suma.
Safu hii pia ilipata fulsa ya kuzungumza na Mkurugenzi wa Nawina Resort, Bi, Mery Komba, ambaye alisema kuwa anamshukuru Mungu kwa hatua aliyoweza kufikia katika kuandaa Burudani katika Ukumbi wa Nawina Resort “ Namshuru Mungu kwa kuwa ameweza kunisimamia katika kuandaa tamasha hili, kwani si kitu rahisi na wateja wangu waendelee kutegemea vitu vizuri zaidi kwani nawapenda wote, na napenda kuchukua fulsa hii kuwakaribisha wakazi wa mbagala na vitongoji vyake katika ukumbi wa Nawina Resort mbagala kuu, kwani tunaendelea kuwaandaliwa vitu vingi vizuri vitakavyozidi kuwapa raha”alisema mary Komba.
Aidha ukumbi huo ambao unapatikana katika Eneo la mbagala kwa sasa umeendelea kuwa gumzo kutokana na maboresho yaliyofanyika baada ya kupata ajali ya moto hivi karibuni.
Kutokana na hivyo umeweza kuboreshwa na kuwa na eneo pana kwa ajili ya usalama, eneo la maegesho Parking za magari, pikipiki na baiskeli.
Kuhusu suala la usumbufu kwa wateja kwa sasa katika ukumbi huo hakuna kwani wateja wanaendelea kupata huduma inayostahili ikiwa ni pamoja na vinywaji na Chakula.
“Natarajia kuendelea kuukarabati ukumbi huu wa Nawina Resort, na matarajio makubwa ni kuwawekea wakazi wa mbagala Ukumbi wa kisasa wenye hadhi ya kimataifa itakayowatikisha watu mbali mbali ususani vijana wa hiki yaani wapenda burudani, (NIGHT CLUB) itakayo kuwa pamoja na ukumbi”aliongeza Mary Komba.
 Hata hivyo aliwataka wapenzi wote wa Nawina kukaribia kila siku kupata vinywaji na chakula vinavyoandaliwa kwa kiwango cha hali ya juu ukilinganisha na maeneo mengine .
Vibao vingine vinavyoendelea kutikisa ndani ya Mashauzi ni pamoja na kibao cha ropokeni yanayowahusu kilichoimbwa na Saida Ramadhani, Haya ni Mapenzi tu kibao kilichoimbwa na Zubeida Malicky, Bonge la Bwana kibao kilichoimbwa na Hashim Saidi.
Burudani hiyo ilianza mapema saa 2:00 usiku na kuendelea.

Mwisho

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni