Jumatatu, 17 Machi 2014

MOYES AENDELEA KULA ZA USO, KOCHA EVERTON APONDA TABIA YAKE YA KUTOPENDA SOKA LA VIJANA!!

Na:Zuhura Masoud, WWW.DACICO FM RADIO.COM
KOCHA wa timu ya vijana ya Everton chini ya miaka 18, Kevin Sheedy ameandika ujumbe mzito katika akaunti yake ya Twite akimkosoa kocha wa Manchester United, David Moyes kuwa  katika maisha yake akiwa Merseyside alikuwa hapendelei kuwatumia vijana wake.
Sheedy  alifanya kazi kwa zaidi ya miaka saba akiwa kocha wa Akademi ya klabu hiyo wakati Moyes akiwa kocha mkuu wa timu ya wakubwa kabla ya kutimkia Man United kurithi mikoba ya Alex Ferguson.
Moyes na Man United yake jana waliangukia pua baada ya kulala kwa kipigo kizito cha mabao 3-0 kutoka kwa majogoo wa jiji, Liverpool, katika dimba lao la Old Trafford
Frustrated figure: Everton Under 18s manager Kevin Sheedy has criticised David Moyes' dealings with the youth team during his time at the club
Kocha wa vijana chini ya miaka 18 wa  Everton  Kevin Sheedy amemkosoa David Moyes kwa kutokuwa na tabia ya kuwatumia vijana
 wakati akifanya naye kazi Everton
Dejected: Moyes looks glum during his side's 3-0 home defeat by rivals Liverpool on Sunday
Kakata tamaa: Moyes akionekana kukata tamaa baada ya kipigo cha mabao 3-0 jana dhidi ya Liverpool
Back at work: Moyes arrives at United's Carrington training complex on Monday morning
 Akirudi kazini: Moyes  akiwasili katika uwanja wa mazoezi wa Man United,  Carrington jana
Game over: Liverpool striker Luis Suarez celebrates scoring his side's third goal as United prepare to kick-off
 Mechi imekwisha: Mshambuliaji wa Liverpool, Luis Suarez akifurahia bao la tatu hapo jana huku mpira ukielekea kumalizika

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni